UANDAAJI WA KITALU CHA MBOGA MBOGA KITAALAMU

                                    Jinsi ya kuandaa kitalu na kuzalisha miche ya mboga mboga

ONION GROUND NURSERY
Bwana Castrory wa Iringa akiandaa kitalu kwa ajili ya nyanya.kitalu ni kidogo kutokana na kaeneo kadogo kalikokuiepo

kitalu cha mbogamboga
kitalu cha vitunguu cha bwana valerian lusasi kikiwa kitaalam kabsa.


· Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.
· Tengeneza tuta la kubwa wa 1m x 2m (ama urefu unaoona wewe kuwa unakufaaa ila tu upana ubaki kuwa 1mita) . Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha
mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hectare moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.
· Weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na
CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye tuta changanya vizuri na udongo.
· Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati
wa kusia ili miche isisongamane.
· Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na mwagiliwa maji. Udongo
unatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.
· Nyasi ziondolewe mara tu mbegu zikiota .
· Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe katika hali ya usafi.
· Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie umri wa kupandikiza shambani
-siku za ukaaji wa mbegu kitaruni inategemeana na aina ya mbegu ama zao.


Kwa utaalam Na mbegu kwa kilimo hiki tuchek kwa +255757808824 ama saringo50@gmail.com
KARBU NORTAN

No comments

Powered by Blogger.